Sauti za Kiswahili
SAUTI ZA KISWAHILI | |
Kitengo | Muundo wa Neno |
Aina Kuu |
|
NAVIGATION | |
Next | Mofimu |
Prev | Shadda na Kiimbo |
a, b, ch, d, e, f, g, h, i, k, l, m, n, o, p, r, s, t, u, v, w, y, z
Kuna aina mbili za Sauti katika lugha ya Kiswahili:
- Irabu
- Konsonanti
Irabu (Vokali)
a, e, i, o, u
Irabu zinapotamkwa, hewa haizuiliwi katika ala za matamshi.
Jedwali lifuatalo litakuonyesha jinsi ya kubainisha vokali kulingana na sehemu ya ulimi inayoachilia hewa, na jinsi midomo inavyobadilika
Irabu | Sehemu ya Ulimi | Midomo |
e,i | Mbele | Midomo imetandazwa |
a | Katikati; ulimi huinuka na kutandaza | Midomo imetandazwa |
o,u | Nyuma | Midomo imevirigwa |
Konsonanti
b, ch, d, f, g, h, j, k, l, m, n, p, r, s, t, v,w, y, z
Konsontanti zinapotamkwa, hewa huzuiliwa katika ala za matamshi ( ulimi na midomo).
Kuna aina mbili kuu za sauti za konsonanti:
- Sauti Ghuna => konsonanti hizi zinapotamkwa, hewa hutikisa nyuzi za sauti
- Sauti Sighuna => konsonanti hizi zinapotamkwa, hewa haitikisi nyuzi za sauti
Jedwali lifuatalo litakuonyesha aina za konsonanti kulingana na mahali zinapotamkiwa na sauti (ghuna au sighuna)
Midomo | Midomo + Meno | Meno + Ulimi | Ufizi | Kaakaa + ufizi | Kaakaa gumu | Kaakaa Laini | Koo | Aina ya Sauti | |
Vipasuo | p d |
t d |
j | k g |
sighuna ghuna | ||||
Vikwamizo / Vikwaruzo | f v |
th dh |
s z |
sh | kh gh |
h | sighuna ghuna | ||
Kipasuo - kwamizo | ch | sighuna | |||||||
Nazali / Ving'ong'o | m | n | ny | ng' | ghuna | ||||
Kitambaza | l | ghuna | |||||||
Kimadende | r | ghuna | |||||||
Viyeyusho / Nusu Irabu | y | w | ghuna |
Vipasuo ( p,b,k,g,t,d )
Hutamkwa kwa kukutanisha ala za kutamkia ili kufungilia hewa na kisha kuiachilia ghafla
- Vipasuo sighuna (p, k, t ) - hutamkwa bila kutikisa nyuzi za sauti
- Vipasuo ghuna (b, g, d ) - hutamkwa kwa kutikisa nyuzi za sauti
/p/ na /b/ hutamkwa kwa kukutanisha midomo katika meno:
- /p/ - papa, pepea, pipi, popo, pua
- /b/ - baba, bebea, bibi, bobo, bubu
/t/ na /d/ hutamkwa kwa kukutanisha ufizi na ncha ya ulimi
- /t/ - taa, tetea, titi, toto, tua
- /d/ dada, doa, dua
/k/ na /g/ hutamkwa kwa kukutanisha nyuma ya ulimi na kaakaa laini
- /k/ - kaka, koko, kuku
- /g/ - gae, gege, gogo, gugu
Vikwamizo ( d f,v,dh,th, s,z,sh,h,gh)
Pia huitwa Vikwaruzo Hutamkwa kwa kukutanisha ala za matamshi na kisha kuachilia hewa kupitia katika mwanya mwembamba
- Vikwamizo sighuna (f,th,s,kh,h,sh) - hewa haitikisi nyuzi za sauti
- Vikwamizo ghuna (v, dh,z,gh) - hewa hutikisa nyuzi za sauti
/f/ na /v/ hutamkwa kwa kukutanisha mdomo wa chini na wa juu na kuachilia hewa kidogo kupita
- /f/ - faa, fee, fua
- /v/ - vaa, vua
/s/ na /z/ hutamkwa kwa kukutanisha sehemu ya kati ya ulimi na kaakaa gumu
- /s/ - sasa, sisi
- /z/ - zaa, zeze, zizi, zuzu
/dh/ na /th/ hutamkwa kwa kukutanisha ncha ya ulimi na meno ya juu
- /dh/ - dharau, dhani
- /th/ - thubutu
/gh/ na /kh/ hutamkwa kwa kukutanisha kaakaa laini na kilimi
- /dh/ - dharau, dhani
- /th/ - thubutu
/h/ hutamkwa kwa kukutanisha kilimi na koo na kuachilia hewa kwa nguvu
- /h/ - haha, hii, huu
Kipasuo-kwamizo: ( ch )
Pia huitwa kituo-kwamizo - Hutamkwa kwa kukutanisha ulimi na ufizi, na kuachilia hewa
- /ch/ - chacha, chechea, choo
Ving'ong'o / Nazali ( m,n,ng',ny )
Hutamkwa kwa kukutanisha ala za matamshi na kuzuia hewa kupitia kinywani; hewa hupitia puani.
/m/ hutamkwa kwa kukutanisha mdomo wa juu na wa chini, ili kuzuia pumzi kupita kinywani
- /m/ - mama, umeme, mimi,
/n/ hutamkwa kwa kukutanisha ulimi na ufizi, ili hewa ipitie puani
- /n/ - nana, nene, nini, nono, nunua
/ny/ hutamkwa kwa kukutanisha ulimi na kaakaa gumu
- /ny/ - nyanya, nyenyea, nyinyi, nyoa, nyunyu
/ng'/ hutamkwa kwa kukutanisha ulimi na kaakaa laini
- /ng'/ - ng'ang'a, ng'oa
Kitambaza ( l )
Hutamkwa kwa kukutanisha ncha ya ulimi na ufizi huku hewa ikipitia kwenye pande za ulimi bila kukwaruza ufizi
- /l/ - lala, lea, lilia, lo! lulu
Kimadende ( r )
Hutamkwa kwa kupigapiga na kukwaruza ufizi haraka haraka kwa ncha ya ulimi.
- /r/ - rai, rarua,
Viyeyusho ( y,w )
Pia huitwa nusu-irabu. Hutamkwa kwa utaratibu kwa kuleta ala za matamshi karibu sana lakini kuachilia hewa bila kuikwaruza.
/w/ hutamkwa midomo ikiwa wazi
- /w/ - wawa, wewe,
/y/ hutamkiwa kwenye kaakaa gumu
- /y/ - yaya, yeye,
Ala za Kutamkia
Hizi ni sehemu za mwili zinazotumika wakati wa kutamkia maneno:
Meno, Ulimi, Midomo, Pua, Chemba cha Pua, Ufizi, Kaakaa gumu, Kaakaa laini, Kimio , Chemba cha Kinywa, Ncha ya ulimi, Bapa la ulimi, Shina la Ulimi, Koromeo, Kidakatonge, Kongomeo, Nyuzi za Sauti, Koo, Njia ya Chakula